Dullonet Tanzania | Polisi yaamua kuongeza nguvu Tarime
Home                   Burudani               Chatroom            Contact Us             About Us                       Maintenance
Copyright @ 2010 Dullonet.com. All Right Reserved
Entertainment News
Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad anatarajiwa kuwasili nchini Zimbabwe hii leo katika awamu ya kwanza ya ziara yake barani afrika.


Ahmadinejad vile vile anatarajiwa kuzuru Uganda wakati wa ziara yake barani Afrika. Mbali na kujadili masuala ya kibiashara na kiuchumi, rais huyo wa Iran anatarajiwa kujadili mpango wa nchi yake wa Nuklia na rais wa Uganda Yoweri Museveni.


Mwaka uliopita utawala wa Teheran ulikataa mpango ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa, ambapo Iran ingepokea mafuta itakayotumika kwenye viwanda vyake vya nuklia ikiwa itasalimisha akiba yake ya madini yaliyorotubishwa ya Uranium.


Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Manouchehr Mottaki, amesema ujumbe wa Iran, utapendekeza mpango mbadala wa mafuta ya viwanda vyake vya nuklia, wakati wa ziara yao katika nchini wanachama wa kudumu katika baraza la usalama la umoja wa mataifa.

Uganda na Lebanon, ni wanachama wa baraza hilo la usalama la umoja wa mataifa.





Posted by Dullonet: 22.04.2010                                                        Source: 
Written by: BBC
Online Radio Live


Dullonet Tanzania Online Instant Chatroom
Dullonet Tanzania Online Music
.............Tanzania Website Network...........
Video za habari na matukio Mbalimbali.