Copyright @ 2010 Dullonet.com. All Right Reserved
WAKAZI wa mji mdogo wa nansio wilayani ukerewe mkoani mwanza hawana maji ya bomba kwa zaidi ya siku nne zilizopita kutokana na sehemu ya kuwashia mitambo ya kusukuma maji kualibika.
Wakuzungumzia tatizo hilo wakazi wa mji huo hasa wamiliki wa nyumba za kulala wageni , migahawa na mahotel wamesema hali ya usafi katika vitegauchumi vyao sio nzuri hali ambayo wanaofu inaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko.
Kwaupande wa wananchi wa kawaida wanaoitaji maji kwa matumizi ya nyumbani pia hali inaendelea kuwa mbaya kwasababu wachuuzi wanaouza maji wanazidi kupandisha bei ambapo troli moja yenye maji ya ujazo wa lita 100 iliyokuwa ikiuzwa sh. 300 hivi sasa inauzwa kati y ash 700 hadi 1000 kutegemea na umbali uliopo kati ya ziwani na nyumbani kwa mteja.
Hali hiyo imewafanya akinamama na watoto kuacha shughuri nyingine na kuonekana kwa muda mwingi wakitafuta maji hasa wakiwa katika misururu mirefu visimani hali ambayo inapunguza uzalisha mali.
Akizungumzia tatizo hilo afisa wa afya wa wilaya ya ukerewe Bw. Sospeter masanga amekili kuwa hali ya usafi katika hospital ya wilaya hiyo, vituo vya afya, zahanati na katika nyumba za kulala wageni na mahotel sio nzuri kutokana na tatizo hilo la maji.
Naye meneja wa mamlaka ya maji ya mji wa nansio NAUWASA ,Injinia Tumaini mugassa amesema tatizo hilo limetokea baada ya kifaa kinachotumika kuwashia umeme katika mitambo ya kusukuma maji kuungua jumapili ya wiki iliyopita.
Hata hivyo amesema tayari ofisi yake imeagiza kifaa hicho kinunuliwe jijini mwanza na kikipatikana kitafungwa na hali ya uduma ya maji kwa wakazi wa nansio itarejea katika hali ya kawaida na kuwataka wavute subila wakati tatizo hilo likitafutiwa ufumbuzi.
Posted by Dullonet: 22.04.2010 Source:
Written by: Jovither Kaijage , Ukerewe
Dullonet Tanzania Online Instant Chatroom
Dullonet Tanzania Online Music
.............Tanzania Website Network...........
Video za habari na matukio Mbalimbali.