Dullonet Tanzania | Polisi wadaiwa kushambulia na kuua raia Dar
Home                   Burudani               Chatroom            Contact Us             About Us                       Maintenance
Copyright @ 2010 Dullonet.com. All Right Reserved
Entertainment News
Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA, Sepp Blatter atakuwa mpatanishi katika mzozo kati ya shirikisho la soka barani Afrika-CAF na Togo.


CAF iliiwekea Togo marufuku ya kushiriki katika mashindano yake yote kwa muda wa miaka minne. uamuzi huo uliafikiwa baada ya Togo kujiondoa kwenye fainali za mashindano hayo yaliofanyika nchini Angola baada ya maafisa wake wawili kuuwawa wakati basi lao liliposhambuliwa kwa risasi katika eneo la Cabinda.


CAF ilidai serikali ta Togo iliingilia kati masuala ya usimamizi wa soka kwa kuiamuri, kikosi chake kujiuondoa kwenye fainali hizo na kurejea nyumbani. Lakini Togo imepinga hatua hiyo na kulishitaki shirikisho la CAF katika mahakama ya kimataifa ya upatanishi CAS iliyoko nchini Uswizi.


Sasa kesi hiyo imesimamishwa huku rais wa Blatter akijitayarisha kufanya kikao cha upatanishi na pande hizo mbili tarehe 7 mwezi ujao.



Posted by Dullonet: 22.04.2010                                                Source: 
Writen by: BBC
Online Radio Live


Dullonet Tanzania Online Instant Chatroom
Dullonet Tanzania Online Music
.............Tanzania Website Network...........
Video za habari na matukio Mbalimbali.