Dullonet Tanzania | Waziri awashutumu maafisa wa TRA kwa wizi
Home                   Burudani               Chatroom            Contact Us             About Us                       Maintenance
Copyright @ 2007 Dullonet.com. All Right Reserved
Entertainment News
Website Designing
We're specialized in developing website's that work. .. More
PC Networking
The Networking  specialises in IT and Network Support ... More
PC Maintenance
PC Repair and Computer maintenance, for the home / business user... More
SERIKALI imewasilisha taarifa ya utekelezaji wa Azimio la Bunge kuhusu uuzwaji wa nyumba za serikali ambapo imeanika ubadhirifu uliofanyika wakati wa shughuli hizo na majina ya watuhumiwa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, baadhi ya nyumba ziliuzwa kwa watu binafsi ambao hawakuwa watumishi wa umma, na watumishi wengine walichukua nyumba zaidi ya moja.

Taarifa hiyo iliwasilishwa bungeni jana na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Hezekiah Chibulunje na kugawiwa kwa wabunge na waandishi wa habari, ili wajiandae kabla haijaanza kujadiliwa bungeni wiki ya mwisho ya Bunge la Bajeti.






Online Radio Live
Watu binafsi waliouziwa nyumba hizo kwa mujibu wa taarifa hiyo ni Ester Chilambo ambaye aliuziwa nyumba kwa thamani ya Sh milioni 21.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wakati wa kuuzwa kwa nyumba hiyo alikuwa mtumishi wa Mipango, lakini wakati wa kusaini mkataba alikuwa amehamia Radio Tumaini, haikufafanuliwa kama nyumba hiyo inarudishwa serikalini au ataendelea kuwa nayo. Mwingine ni Mussa Joseph ambaye aliuziwa nyumba iliyopo Ubungo Camp kwa thamani ya Sh milioni 1.5.

Hata hivyo, mteja huyo wa serikali alipokabidhiwa barua ya kusitisha mkataba, alifungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania na hata aliposhindwa kesi, alikata rufaa na shauri lake liko mahakamani bado. Pia yumo Stanley Manongi, ambaye aliuziwa nyumba iliyopo Ubungo Camp kwa Sh milioni 13 ambaye amesharejeshewa fedha zake na nyumba hiyo amepewa mtumishi mwingine wa umma.

Wa mwisho katika kundi la watu binafsi waliouziwa nyumba za serikali ni Monica Senga, ambaye aliuziwa nyumba iliyopo Charambe Upanga kwa Sh milioni 14. Hata hivyo pamoja na mteja huyo kukubali kufutiwa mkataba, serikali imependekeza apangishwe katika nyumba hiyo kibiashara, kwa vile ameifanyia matengenezo makubwa hivyo bado anaishi katika nyumba hiyo.

Taarifa hiyo pia iliwataja watumishi waliouziwa nyumba zaidi ya moja kinyume na utaratibu, akiwamo Dk. Edna Moses, Veronica Mabula, Switbert Bajuza na Agnes Chamshama. Pia ilitaja majina ya watu ambao katika familia moja walinunua nyumba mbili au zaidi. Familia hizo ni ya Ben na Dk. Edna Moses, familia ya Hussein Abdulrahman na Mwanamtama Marandu ya Emil Kayega na Emerensiana Kayega na ya Clement na Esther Mshana.

Familia nyingine ni ya Dk. Jacob na Theodora Mollel na ya Ngore na Zainab Kondo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, nyumba nyingine zilizouzwa kinyume na utaratibu ni pamoja na zilizoko kwenye kambi za Jeshi. Nyingine ni nyumba za taasisi, zilizouzwa kwa watumishi wa Serikali Kuu na ambazo zilikuwa katika maeneo nyeti ya Serikali ambazo ziliuzwa kwa watumishi wa Serikali.

Taarifa hiyo ambayo ilitaja majina ya kila aliyenunua, ilifafanua kuwa baadhi zilirudishwa na baadhi hazijarudishwa kutokana na kuwa na kesi mahakamani. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika makadirio ya matumizi ya Wizara ya Miundombinu ambayo ilisitishwa kuhitimishwa jana kutokana na mahitaji ya kuifanyia mabadiliko makubwa, kulikuwa na Sh bilioni 1.5 zilizotengwa kwa ajili ya kulipa fidia za nyumba zitakazorudishwa serikalini.























.

Posted by Dullonet: 03.07.2009                                                                                                 Source:
Written by: Mwandishi Wetu, Dodoma